Ziwa Victoria (pia: Viktoria Nyanza, Ziwa Nyanza) ni ziwa kubwa Afrika, pia ni chanzo cha mto Nile, hili ni ziwa la pili kwa ukubwa Duniani. Ziwa la kwanza ni Ziwa Superior ambalo lipo Amerika ya Kaskazini. Ziwa Victoria lipo futi 3,726 kutoka usawa wa bahari na lina eneo la maili za mraba zaidi ya 26,000. Maji ya ziwa Victoria yanamiminika kwenye mto Nile na kuelekea bahari ya Mediterenia kwa umbali wa maili 4,000. Ziwa Victoria limekuwa ni kiunganisho na mpaka kwa nchi tatu za Afrika ya mashariki ambazo ni Tanzania, Kenya na Uganda.