Piramidi za Giza

Piramidi za Giza ni kati ya majengo yanayojulikana zaidi duniani. Pamoja na mava mengine ni sehemu ya makaburi ya Giza yaliyokuwa mahali pa kuzika wafalme wa Misri na wakubwa wa milki yao kwa muda wa miaka 2500.

Ziko kando ya bonde la mto Nile, karibu na mji wa Giza takriban kilometa 15 kutoka Kairo, mji mkuu wa Misri.

Historia ya maeneo ya makaburi ya Giza kwa jumla

Makaburi ya kwanza yalijengwa huko tangu chanzo cha milki ya Misri ya Kale takriban miaka 3,000 KK.

Wakati wa nasaba ya 4 ya Misri eneo la makaburi hayo liliongezeka sifa kwa sababu wafalme Kheops, Khefren na Mykerinos waliamua kujenga huko piramidi kwa ajili ya makaburi yao wenyewe.

Kutokana na ujenzi wa makaburi ya kifalme ndugu wa familia zao na maafisa wa juu walizikwa huko pia hadi mwisho wa nasaba ya 7 ya Misri.

Baada ya hapo na kwa sababu ya kuhamishwa kwa mji mkuu wa milki kwenye kusini ya nchi umuhimu wa eneo la makaburi ya Giza ulipungua. Mazishi ya maana yalitokea tena wakati wa nasaba za mwisho za Misri, katika vipindi vya kuvamiwa na Uajemi.

Piramidi kubwa na Sfinksi

Eneo la makaburi ya Giza hujulikana hasa kutokana na piramidi kubwa pamoja na sfinksi kubwa zilizokuwa maarufu tayari katika nyakati za kale. Mwanahistoria wa Ugiriki wa Kale aliyeitwa Herodoti alizihesabu kati ya Maajabu Saba ya Dunia na tangu siku zile miaka 2,500 iliyopita zilitembelewa na watalii.

Piramidi tatu kubwa zinajulikana kufuatana na majina ya Kigiriki ya mafarao au wafalme wa Misri waliozikwa ndani yao: piramidi za Kheops, Khefren na Mykerinos. Piramidi za Kheops na Khefren ziko karibu kimo moja, ile ya Kheops ni kubwa kidogo lakini ile ya Khefren inaonekana kubwa kwa macho kwa sababu imejengwa juu ya ardhi ya juu kiasi kwa hiyo kwa macho ya mtazamaji inafika juu zaidi.

Jina la Kigiriki Jina la Kimisri Alitawala mnamo Kimo asilia Kimo cha leo Kipimo cha
upande wa msingi
Piramidi ya Kheops Khufru ~ 2620
- 2580 KK
146.1 m 138.75 m 230 m
Piramidi ya Khefren Khafre ~ 2558
-2532 KK
143.6 m 136.4 m 215.25
Piramidi ya Mykerinos Menkaure 2558
-2532 KK
65.55 m 62 m 102.2 m
x 104.4 m

Piramidi hizo zote hazikukaa peke yake bali zilijengwa pamoja na majengo ya kando.

  • Kila piramidi ilikuwa na mahekalu mawili ambako makuhani walitoa sadaka kwa ajili ya roho za mafarao marehemu peponi. Hekalu 1a kwanza lilijengwa mbali kidogo, kwenye chanzo cha barabara ya maandamano yaliyoendelea hadi hekalu la pili karibu na piramidi. Njia hizo za maandamano zilitumiwa hasa wakati wa sherehe za kumkumbuka farao.
  • Kwa kawaida malkia (wake wa farao) walizikwa katika piramidi ndogo au makaburi mengine kando ya piramidi kubwa. Piramidi za Kheops na Mykerinus huwa na piramidi 3 za malkia wa kila mfalme. Kwenye piramidi za Khefren hakuna makaburi ya malkia yaliyotambuliwa.

Historia ya baadaye

Tangu siku za kale watu walichukua mawe kutoka majengo ya Misri kwa kuyatumia katika majengo ya nyakati zao. Hii ndiyo sababu ya kwamba kimo cha piramidi kimepunga na hasa mawe mazuri yaliyofunika nyuso za piramidi yamepotea.

Katika karne ya 12 BK mtawala wa Misri al-Malek al-Aziz Othman ben Yusuf alijaribu kubomoa piramidi akizitazama kama ushahidi wa upagani wa kale. Wafanyakazi walianza kukata mawe kutoka piramidi ndogo ya Mykerinos lakini ikaonekana ya kwamba kazi ya kubomoa labda ingekuwa ghali sawa na kujenga. Baada ya miezi kadhaa shughuli hizo zilisimamishwa na hadi leo kuna pengo katika ukuta wa kaskazini.

Viungo vya Nje

Imeorodheshwa katika kategoria zifuatazo:
Tuma maoni
Vidokezo na Vidokezo
cxbyte
29 May 2012
vrlo lijep
cxbyte
29 May 2012
Très belle
cxbyte
29 May 2012
Very nice
cxbyte
16 May 2012
что не очевидно?
Vadim I
16 May 2012
Теперь поздно, с новой властью к туристам не очень-то хорошо относятся =]
Dave Mc
27 August 2018
The pyramids don't look that far from the road, but they're actually are really far, they're just wicked big so they look closer than they actually are. The camel tours are expensive, but worth it!
DoubleTree by Hilton
If you are a horse riding lover visit FB Stables and Ride in the shadow of the Great Pyramids or further afield on a half day trip to Saqqara or Abu Sir or camp out over night with a barbecue and fire
Dave Mc
27 August 2018
The pyramids a really, really huge. You might think about climbing one, but once you get there, you'll change your mind!
Dave Mc
27 August 2018
The pyramids are really a must see, bucket list item. If you have the opportunity, you definitely have to do it.
David Ladera
21 May 2018
I would recommend to avoid crowded hours even if the weather is hot to have a better experience. Camel tours are 100 EGB / 30 min / 1 person
Veysel Soylu
2 March 2017
It's amazing to visit pyramids at the age of thousands... No words enough to describe them. Get rid of people who asking money from you all the time
Pakia maoni zaidi
foursquare.com
Marriott Mena House, Cairo

kuanzia $247

Four Seasons Hotel Cairo at The First Residence

kuanzia $180

Swiss Inn Nile Hotel

kuanzia $29

Barcelo Cairo Pyramids

kuanzia $60

Amarante Pyramids Hotel

kuanzia $34

Hor Moheb Hotel

kuanzia $31

Vitunguu vilivyopendekezwa karibu

Ona yote Ona yote
Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Pyramid of Khafre

The Pyramid of Khafre is the second largest of the Ancient Egyptian

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Khufu ship

The Khufu ship is an intact full-size vessel from Ancient Egypt that

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Piramidi za Giza

Piramidi za Giza ni kati ya majengo yanayojulikana zaidi duniani.

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Sfinksi

Sfinksi (kwa Kiingereza sphinx) ni kiumbe cha visasili katika tamaduni

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Pyramid of Menkaure

The Pyramid of Menkaure, located on the Giza Plateau in the

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Layer Pyramid

The Layer Pyramid (known locally in Arabic as il-haram il-midawwar,

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Abu Rawash

Abu Rawash (also known as Abu Roach, Abu Roash), 8 km to the North of

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Pyramid of Djedefre

The Pyramid of Djedefre consists today mostly of ruins located at Abu

Vivutio sawa vya watalii

Ona yote Ona yote
Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Piramidi za Giza

Piramidi za Giza ni kati ya majengo yanayojulikana zaidi duniani.

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Pyramid of Djoser

|Owner=Djoser

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Philopappos Monument

The Philopappos Monument (Greek: Μνημείο Φιλοπάππου) is an ancient Gr

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Pyramid of Amenemhat III (Dahshur)

King Amenemhat III built the Black pyramid during the Middle Kingdom

Ongeza kwenye orodha ya matamanio
Nimekuwa hapa
Walitembelewa
Red Pyramid

The Red Pyramid, also called the North Pyramid is the largest of the

Tazama maeneo yote yanayofanana