Pelé (jina lake halisi ni Edison Arantes do Nascimento; amezaliwa mwaka 1940) alikuwa mchezaji wa mpira wa miguu kutoka Brazili. Anahesabiwa na wengi kuwa mchezaji mzuri zaidi wa wakati wote.
Alicheza kama mshambuliaji wa kati. Akiwa na miaka 17 tu aliisaidia Brazili kutwaa kombe la dunia 1958, na baadaye 1961 na baadaye tena mwaka 1970. Aliweka rekodi mwaka 1958 ya kuwa mchezaji mdogo kuliko wote duniani kucheza katika fainali ya kombe la dunia alipocheza akiwa na umri wa miaka 17. Alivuma sana katika miaka ya 1970 duniani kote.
Alifunga mabao zaidi ya 1000 katika kipindi cha uchezaji wake kabla ya kustaafu.